Kwenye Swahilies kuna vipengele vikuu 3 ambavyo ni “Market”, “Goals” na “Learn”.Tumeelezea muongozo wa kila kipengele hapa chini;
Market
“Market” ni kipengele cha masoko ambacho kinakuwezesha kununua bidhaa mbalimbali kwa kulipa kidogo kidogo, muongozo na masherti ya kipengele hichi ni yafuatato;
- “Lipia Yote” ni malipo yaliyokamilika ya bidhaa husika ndani ya wakati uliopo. “Lipa Mdogomdogo” ni malipo ya awamu ambapo kila bidhaa ina muda wake wa kikomo wa kulipia ambao umeandikwa kwenye maelezo ya kila bidhaa.
- Kumbukumbu za malipo yako ya “Lipa mdogomdogo” zipo upande wa kushoto wa application hii kwenye “menu” kipengele cha “orders” ambapo utaweza kuona muenendo wa manunuzi yako yote kama kiasi ulicholipa kwa kila bidhaa na kiasi kilichobaki kukamilisha malipo ya kila bidhaa uliyoanza kuilpia.
- Kiasi cha chini kuanza kulipa au kuendelea kulipa kwenye “Lipa Mdogo Mdogo” ni 1,000 Tsh.
- Ukishindwa kukamilisha malipo ya bidhaa ndani ya wakati uliopangwa, utalazimika kuchagua bidhaa nyingine kwenye application ya Swahilies ambayo inathamani ya malipo uliyofikia kwa wakati huo.
- Tofauti na bidhaa kama suti na bidhaa za kutengenezwa kama vitanda, bidhaa zingine zote wenda unalipa sasa “Lipia yote” ****au unalipa kwa awamu “Lipa Mdogo mdogo” bidhaa yako itakufikia ndani ya masaa 24 baada ya kukamilisha malipo ya bidhaa husika(kwa wakazi wa dar tu).
- Una haki ya kubadilishiwa bidhaa ndani ya siku 7 kama bidhaa uliyoinunua umeikuta na dosari au iko tofauti na ambavyo ilielezewa wakati unainunua kwenye application hii ya Swahilies.Una nafasi ya kurudishiwa pesa yako endapo bidhaa uliyoinunua umeikuta na dosari na kampuni ya Swahilies imeshindwa kukupatia mbadala wa bidhaa ambayo umeikuta na dosari.
- Una haki ya kughairisha kuendelea kununua bidhaa ambayo umeanza kulipa “mdogo mdogo” na kuamuru pesa yako ihamishiwe kwenye bidhaa nyingine.
- Kumbuka kujaza taarifa na mawasiliano ya mtu wako wa karibu kwenye kipengele cha “Extral information” ili tuweze kuwasiliana na mtu wako wa karibu siku tukishindwa kuwasiliana na wewe ukiwa umepata dhalula au umetoweka bila kufikishiwa bidhaa yako.
Goal
“Goals” ni kipengele kinachokuwezesha kujiwekea malengo ya kulipia kidogo kidogo bidhaa na huduma mbalimbali ambazo hata hazipo ndani ya Swahilies.zingatia mambo yafuatayo kwenye kipengele hichi cha “Goals”
- “Goals” ni huduma ya kujiwekea malengo ya kulipia kidogo kidogo huduma au bidhaa kupitia Swahilies, “Goals” sio sehemu ya kutunza pesa(savings) bali kulipia huduma au bidhaa kidogo kidogo.